Ashukuriwe, Bwana Mungu wetu, aliye tuumba sote tukawa watu
wake, Mungu wa upendo, Mungu wa huruma, Mungu wa rehema, asiye mwepesi wa
asira, Mungu mvumilivu anaye tu vumilia akijua sisi tu wadhaifu, Mungu aokoaye
yaani nasiye tuacha tupotee, Mungu anayetuwazia mema,.
Sifa na utukufu, na heshima, na adhama, na uweza, na nguvu,
na mamlaka, na enzi zina yeye tokea mwanzo, sasa na hata mimlele.
Shukrani, na utiifu wote, na heshima,zote na ibada ya mioyo
ya wanadamu aliyowakomboa pamoja na viumbe vyote viwezavyo kumsifu katika hili
kwamba ametuokoa na mauti, tuwe wake, sifa hizo na shukrani na zote anayo
stahili zimrudie sasa hata milele.
Ashukuriwe Bwana wetu Yesu Kristo aliye jitoa nafsi yake na
kutifia msalabani ili kutuokoa na adhabu ya mauti iliyo tu kumba kwa sababu ya
dhambi zetu,aliacha utukufu na heshima yake akaja kutupenda tulio kua
hatumpendi, kututafuta tilokua hatumtafuti, kutuita tulio kuwa hatumsikilizi .
Hata kutimiliza ukombozi na kututoa katika nguvu za giza
zilizo tufunga na kutufanya watumwa,tukifungwa kwa minyororo tusiyo weza
kuvunja, tukitumikiswa katika dhambi na kuteswa sana.
Yeye kwa damu yake
amelipa deni ya hatia yetu, na gharama ya adhabu yetu aliichukua mwilini mwake
,akituita marafiki na ndugu zake, akafa, tgena kifo cha aibu ili ntuheshimike,
akafanyika laana ili kututoa katika laana na ametutoa kweli kweli tu kawa huru.
Ashukuriwe Roho mtaka tifu, akamilishi wa utakatifu wetu,
mwalimu wa kweli, kiongoze mwema, atufanyaye tupendeze na kuzidi kumpendeza
Munmgu baba.
TUJUE TUKISEMA KRISTO AMETUKOMBOA AMETUTOA WAPI NA KUTUWEKA
WAPI.
Ndugu wapendwa wote twajua kwamba kwa mtu mmoja dhambi
iliingia duniani na mauti ikatawala wote tukawa wenyedhambi kwani tulizaliwa
chini ya chambi, yaani kutoka kwa Adam na tukaishi maisha ya dhambi tukitenda
dhambi,{Mwanzo 3:19;Rumi 5:12,14}.
Katika hili yaani kabla ya kutakaswa mtu asemaye hana dhambi
anajidanganya mwenyewe,kwani sote tume tenda dhambi{1Yohana 1:8,1o}.
Tujue kwamba sote tulifanya dhambi na kupungukiwa katika
utukufu Mungu {Rumi 3:23}
Tulikuwa tukitumikishwa
chini ya laana huku tukiangaika usiku na mchana tukilia kwa mateso ya dhambi na
kubeba mizingo ya laana ipatikanayo na dhambi walizo fanya babu zetu ambao
wengine hawapo nasisi tukaendeleza hata kufanya machukizo pengine kuliko wao.
Haya ni maisha ya dhambi wakati wote ambao mtu haja kutana
na neema ya Mungu.
NAMNA GANI MUNGU ANAFUTA DHAMBI ZETU NA LAANA ILIYOKUA JUU
YETU?
Mungu wa upendo alimtuma Yesu Kristo ambaye ametuokoa yeye
kwa damu yake na kufuta dhambi zetu zote,yaani ni zote,
Baada ya mtu kuungama dhambi zange Mungu ni mwaminifu katka
Kristo yetu anamfutia mtu huyo dhambi zake zote yaani sio nusu {Zab 103:3; Isaya
33:24, 1Yohna1:9}.
Taratibu ya Mungu ikowazi kwamba mtu akighahiri akaacha uovu
na kutenda mema akufuata maagizo ya Mungu ,dhambi zake zote zinzfuta na wala
haita kumbukwa hata moja{Ezekiel18:21,22; 33:15,16}.
Bora tuelewe kwamba dhambi zote zinasafishwa na mtu
kusamehewa mara moja haijalishi ilikua ni dhambi za nani au zilikua kubwa kiasi
gani hakuna dhambi yenye gharama kubwa kuliko damu ya Yesu kwamba ikifutwa bado
inaonekana.
BAADA YA KUSAFISHWA DHAMBI ZETU JE TUNAKUA NA MAISHA GANI
Ndugu zangu ,wote walio kwisha kuoshwa katika damu ya mwana
kondoo nakukombolewa wanakua na sifa hizi.
1.Wana hesabiwa haki ipatikanayo kwa njia ya imani yaani
bure kwa neema ya Mungu Baba kwa njia ya
ukombozi ulio katika Kristo Yesu{Rumi 3:22,24,25,Galatia 2:16}.
2.Tuna kuwa viumbe vipya,yakale yamepita, tulio vaa upya
sura na mfano wa muumba wetu{2Korintho 5:17}.
3.Tuna kuwa wana wa Mungu kwa kuzaliwa kupitia Kristo Yesu,
{Rumi8:16, 1Yohana 3:1}.
4.Sisi tu uzao mteule, kuhani wa kifalme watu wa ukoo wa
watakatifu.Watu wasio na laana.
Ndugu zangu ikiwa tumetakaswa kwa damu yake yeye aliyetufia .
TUMEKOMBOLEWA NA KUTAKASWA KWA DAMU YA KRISTO TUNA KUWA
HATUNA TUMEKOMBOLEWA NA KUWEKWA HURU KWELIKWELI
Kama asemavyo mahali Fulani kwamba , mwana akikuweka huru
unakuwa huru kwelikweli{Yohana 8:36}.
Hapana hukumu ya adhabu juu yao hao walio katika Kristo
Yesu{Rumi 8:1,2}.
Ndugu zangu ni bora tulijue ukweli kwamba , Mungu mwenyewe
alisema , kila mtu atakufa kwa dhambizake mwenyewe, baba hata beba dhambi ya
mwanaye wala mwana hata beba dhambi ya baba yake au mama yake,ila nafsi
itendayo dhambi ndiyo itakayo kufa{Ezekieli 18:2-20}.
Watu wamenga’nga’nia andiko bila kujua Mungun alishanena
katika agano jipya akisema atafanya agano jipya sio kama aliyo fanya na babu
zetu,{Yeremia 31:31,32}.
Wakati wa agano jipya Mungu aliongelea akisema mtu hatasema 3
wamekula Zabibu kali na watoto ndio meno yao yana kufa ganzi, la! Hasha!
,Kalamtu atakufa kwa dhambi zake mwenyewe, kila mtu alaye Zabibu kali meno yake
yatakufa ganzi mwenyewe{Yeremia 31:29,30}.
Ndugu zangu wapendwa unaposoma maandiko jitahidi uweze
kuelewa yafuatayo:
[A] Unayoya soma ninani aemeyasema, yaani nani uliongea
hapo.
[B] Walengwa ni wakina nani yawezekana hata sio wewe au sio
hao unao waambia.
[C] Neno unalolisoma ilikua litimie kwa majira gani au
ilikua ni ya nyakati gani, je wakati uliopita? Au wakati uliopo? Au ni kwa
wakati ujao?.Na wewe ujue unlisoma ukiwa katika wakati gani.
[D] Ujue kusudi la neon ulisomalo, kwama lilikusudia nini
haswa.
[E] Ujue kama neno hilo lakufaa wewe au sio lako.usipoteze
mda wako kuangaika na lisilo lako.
[F] Ji ulize kwamba ,je unayaelewa hayo unayo yasoma?.
Unajua watu wame hubiriwa,wametabiriwa, nakufundishwa habari
zisizo zakwao yaani yasiyo wahusu kabisa na kubebeswa mizigo mizito na wameacha
mambo ya misingi inayo wahusu hata badala ya watu wa Mungu kuendelea mbele
wamekua wakiishi kwa hofu isiyo kua ya kawaida.
Sipati picha mtu anaambiwa atoe sadaka ya ukombozi yaani
itakayo kuwa na nguvu kuliko alizo toa babu yake kwa kwenye madhabahu ya
Shetani.Kwani hamja soma kwamba Yesu alijitoa sadaka kwa damu yake takatiofu
iliyo zaidi ya damu nya wanyama, yeye amekua dhabihu na sadaka ya kuondoa
dhambi?.
Unajua Mungu angeona kama ukombozi sadaka yake yafaa
kufanyika kwa kutoa fedha ,au kondoo,au mbuzi yaani asingemtuma Yesu aje kwani
kabla hajamtuma vyote hivyo vilikuwepo duniani,
Hebu tutokane na mafundisho ya watu wasioijua siri ya Mungu
japo wanayasoma habari hizi kila siku lakini masikio ya roho zao zimejaa
michanga na kuzibwa na lami wasi sikie wala kuelewa.
Mtu anakuambia utowe sadaka kwa ajili ya kukomboa wazaliwa
wakwanza .wakati Yesu alijitoa yeye
aliye mzaliwa wa kwanza kwa viumbe vyote, ili akomboe uzao wote ya wanadamu na
hata wanyama walio kua wakitolewa akawa limbuko isiyo toliwa kwa mikono ya
wanadamu.
Nikweli kwamba Munmgu alisema atapitiliza laana kwa kizazi
wasio mpenda hata kizazi cha nne {Kutok 20:5; Kumbukumbu 5:9}, wakati anampa
Musa sheria katika agano la kale, lakini yeye mwenyewe amesema , ataleta agano
jipya na ameleta tena ya neema ambayo juu yake ameahidi kumlipa kila mmoja
kadri ya matendo yake.
Mtu atakula matunda ya matendo yake, {Isaya 3:10}.
Kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe,{Galatia 6:5}.
Kila mtu atatoa hesabu ya matendo yake mwenyewe mbele za
Mungu{Rumi 14:12}.
Kumekuwepo na mafundisho ya
aina fulani yanayo wafanya watu wachanganyikiwe na wazidi kujihukumu
nafsini mwao nakuona kama ile neema ya wokovu walio upata haina maana.
Ikiwa mtu yu ndani ya Kristo amekua kiumbe kipya nay a kale
yamepita na wala hauhukumiwi kwa makosa
ya mtu yeyote hata kama ni baba yake wala habebi laana ya aina yoyote!
Siku hizi imekuwaje? Mtu anaambiwa atafanyiwa ukombozi atoke katika laana ya
vizazi wakati a mesha mkombolewa na kusafishwa kwa damu ya Kristo?
Imekuweje mtu anaambiwa aingiye kwenye maombi ya kufunga ili
nabii au mtume akamkomboe kutokana na laana fulani fulani, wakati mtu huyu
amemwamini Kristo na tiyari yu ndani ya Kristo ahesabiwi dhambi wala hana laana
juu yake?.
Aliye waambia mtu anasamehewa dhambi na kukombolewa nab ado anabaki
na laana ,ni nani?.
Hauna nabii wala mtume wala mtu awaye yote ambaye Mungu
alimpa ruhusa au uweza wa kuondoa laana isipokua Kristo, hayo hayaondolewi kwa
maombezi bali ikiwa mtu amemwamini Kristo na akampokea naye anapata neema ya
wokovu na Kristo kuingia nnadani yake, dhambi na laana zinafutwa mara moja wala
hazi kumbukwi tena.
Alipo sema watakatifu wazidi kujitakasa inamaana wazidi
kudumu katika utakatifu na kutenda yaliyo matakatifu, wasirudi wakaji najisi,
wakae ndani ya Kristo atutakasaye wakati wote kupitia roho wake akaaye ndani
yetu ili tuzidi kumpendeza Mungu kila itwapo leo’
Watu wamekuwa wakiyumba yumba huku nahuklu mara wakimbie kwa
huyu au kwa Yule, wakisikia matangazo kwamba wataondolewa laana, mikosi, na
mengine mengi, huku anasema Yesu yumo ndani yake, labda nisema watu hawajajua
vile Yesu amefanya maishani mwao.
Shetani naye akishaona watu hawajaelewa kama wamesha wekwa
huru, amezidi kuwatumia manabii wake ili kuwaita kwa namna nyingine awakamate
fikra na kuwatesa tena awazuia wasiijue kweli.
Nisikilize vizuri, watu wasitake kuwahisha maisha, na tama ambayo
imewafanya wengi waingie majaribuni, ikiwa umeokoka sio kwamba ndio siku hio
unakua tajiri hapana , bado unahitajika, kufanya kazi na kubudi miradi ya
kukuingiozia kipato .
Sio kwenda kutafuta maombi ukisema ya wezekana ni laana ya
vizazi, wewe ahauna laana Yesu amesha kuweka huru fanya kazi tu kwa bidii na Mungu ataibariki kazi ya mikono
yako.
Pengine mtu alikua akifanya dhambi ya aina fulani ndo apate
hiyo pesa ya utumwa unapo amua kuiacha dhambi hiyo, usifikiri utapata fedha
zile maana uananza maisha mapya kuwa na subira.
Pengine wewe umeokoka na unaona kwa upande wa uchumi hauko
vyema , hiyo sio laana yaweze kana tu wakati wako wakupata hauja fika ndugu
yangu an ikifika utafurahi tu.
Mkumbukeni Irahim na Sara mkewe walivyo kuwa wakimwamini
,Mungu lakini waliishi miaka mingi bila
kua na motto, je utasema walikua na laana? Kama ndiye angekua katika nyakati
zetu hizi , naisi kila siku manabii waleo wangemtabiria mengi na kumsumbua na
maombi mpaka basi, tena wengine wangemwambia kuna uchawi alimezeshwa ndio
imemzuia asipate motto mjika tisni sio michache, wewe unamiaka mingapi
ukingojea ahadi ya Bwana.
Ndugu zangu Bwana Mungu wetu ni mwaminifu yeye ataya timiza
yote aliyo tu ahidia.
Nikwambiye ukweli kwamba , ikiwa Mungu ameku ahidi atakupa
kitu acha kuangaika atalkupa tu usijidanganye ukisema kwamba Shetani anaweza
kuzuia chocho alicho panga Mungu, hawezi kuchelewesha wala kuzuia kwani hana
uwezo huo.
Ukiona inachelewa ujue wakati ulio klusudiwa bado lakini
mwamini Mungu kuwa ni mwaminifu atayatimiza
ahadi zake kwako yeye asiye sema uonga hata acha kutenda alicho sema.
Usiache kuangaika , mara ufanye nini, usipende kumtaja taja .
Shetani kinywani mwako wewe kila kitu Shetani hata kama Mungu akiona sio wakati
un aofaa wewe kukupatia kitu fulani atakupa kwa wakati mwingine mara umesha
kimbilia kusema Shetani, mnatukuza bila kujua na kuonyesha vile mnavyo mwogopa.
Usipende kutangaza shida ulio nayo Bali tangaza ukuu wa
Mungu wako na kupuuza kelele za adui.
HEBU WEWE JIULIZE, AKIJA NABII HUYU ATAKUAMBIA TUNAENDA KUOMBA KUVUNJA
LAANA YA ZIZAZI, AKIJA HUYU MARA TUAENDA KUKUFANYIA UKOMBOZI NA UZAO WAKO,
AKIJA HUYU MARA TUNAENDA KUKUTOA WALIKO KUZIKA WACHAWI , AKIJA HUYU NA YULE NA
YULE NA YULE HIVYO HIVYO MIAKA INAENDA
UKO NDANI YA IMANI JIULIZE KWAMBA.
HIZO NI LAANA ZA NAMNA GANI AMBAZO HAZIISHI NA KAMA KILA MWAKA TANGU
UMEMWAMINI KRISTO UNAVUNJA NA KUKOMBOLEWA TU KWANI HIZO ZINAONGEZEKA KILA MWAKA
UA NDO ZIKO PALEPALE?.
SWALI LINGINE JIULIZE IKIWA YESU ALISHA KUFA MIAKA MINGI ILIOYO PITA NA
WEWE UMEMWAMINI NA ALISEMA YOTE YAMEKWISHA HAYO UNAYO AMBIWA YANA TOKA WAPI?.
WEWE KAMA UNA AMBIWA UVUNJE YA MAKOSA YA BABU, KESHO YA BIBI, KESHO
KUTWA YA MAMA, SIKUINAYO FUATRA YA BABA, UTAWEZA HIZO AU UTAISHI NA KUTOKA
DUNIANI HAUJAZIMALIZA? NA KAMA UTAKUA HAUJAZI MALIZA UKAFA AU YESU AKAJA HAQUJA
MALIZA KUVUNJA MADHA BAHU ZA KISHETANI NA LAANA HIZO , UNADHANI UTAINGIA KATIKA
UZIMA WA MILELE KWELI UKIWA NA HIZO LAANA?
MBONA TWAJIBEBESHA MIZIGO ISIYO YETU?.
KAMA UNAJU UMESHA KOMBOLEWA NA
KUSAFISHWA KWA DAMU YA MWANA KONDOO TANGAZA UKO HURU, ISHI KWA AMANI KWAMBA
HAUKO MCHINA YA LAANA, WAZUIE WANAO KULETEA HABARI ZISIZO ZAKO HATA AKIKUAMBIA
MUNGU AMEMWAMBIA UNALAANA NA WEWE UNAJUA YESU ALISHAONDOA LAANA ZOTE MWAMBIE
POLE TENA MWELEZE WEWE NI KIUMBE KIPYA HABARI HIZO NI ZAMANI ZILE WALA
HAZIKUHUSU WEWE.
NDUGU ZANGU TUJUE KWAMBA WALA
HAKUNA HUKUMU YA ADHABU JUU YETU SISI TULIO KATIKA KRISTO YESU.
NEEMA YA MUNGU BABA NA UPENDO WA
YESU KRISTO NA USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKANASI SASA HATA MILELE AMINA.
Kwa maswali au maoni usisite kuwasiliana nami,
Ochiein gomeno@gmail.com,
No comments:
Post a Comment