ROHO MTAKATIFU

ROHO MTAKATIFU  NDIYE MKAMILSHI WA WOKOVU WETU

Ndugu mpendwa  kabla hatujaendelea  kwa habari za Roho mtakatifu nivyema tuelewe kwanza mambo yafuatayo.Yaani kuweza kujibu maswali ya muhimu yawezayo kutufanya  tuelewe  kuhusu huyo Roho   mtakatifu .Kama,
i.         Nini maana  ya Roho
ii.       kuna aina ngapi za  Roho
iii.      Nini maana ya Roho mtakatifu
iv.     Kuna aina ngapi za Roho mtakatifu
Roho ni nguvu au sehemu ya uhai ya asili itendayo kazi pasipo onekana kwa macho ya kawaida katika ulimwengu wa nyama .Ni nafsi hai itendayo kazi pasipo onekana kwa macho ya nje .kwa jina jingine pumzi ya uhai  iliyo toka kwa Mungu.
Hapo mwanzo Mungu alipo muumba mtu akampulizia pumzi ya uhai puani mtu akawa nafsi hai[Mwa 2:7].
Kuna aina nne  za roho, nazo ni
I.        Roho ya mwanadamu.
II.      Roho ya wanyama na viumbe vingine hai.
III.    Roho ya shetani[roho chafu].
IV.    Roho  wa Mungu [mtakatifu].
Ndugu yangu mpendwa napenda nikujulisha kuwa, kila unacho kiona kina uhai katika Dunia hii  ina roho kwani,  Mungu ndiye aliye  toa pumzi yake ya uhai akawapa  viumbe vyote  hio sehemu  ya uhai aliyo nayo ,yeye ndiye aliye toa pumzi yake ya uhai akaituma kwa viumbe alivyo vipangia  kuwa na  uhai navyo vikawa hai .Uhai tulio nao ni sehemu ya pumzi ya  Mungu ambayo ametupa na hiyo pumzi ni roho wake atendaye kazi Duniani hata sasa.

ROHO YA  MWANADAMU

Bwana Mungu akamuumba Mtu kwa mfano wake kwa sura yake mwenyewe,lakini baada ya  kumuumba kwa mavumbi ya ardhi , alimpulizia pumzi ya uhai  puani mtu akawa nafsi hai[Mwa 2:7] .
Mtu amegawanyika katika sehemu kuu mbili nazo ni; mwili na roho aliye tangulia ni mwili ndiye alikuwa wakwanza halafu wapili ni roho  ,kwani  alifinyanga  na kuumba kwanza kwa mavumbi ya ardhi ndipo alipo weka roho yake kwa kupitia puani alipo mpulizia pumzi puani.
Mtu wa asili wa kwanza yaani mwili ulio tokana na mavumbi ya ardhi mwisho wake ni udongo hauendi kokote bali uzikwa na kurudi uliko toka na pumzi ya uhai yaani  roho, nayo humrudia mwenye kuitoa[Mhub 12:7; Ayub 34:14--16; 1Kor 15:40--49].
Kuna utofauti kidogo kati ya moyo na roho  kwani kwenye moyo ndipo Mungu alipo iweka  Roho yake ,moyo ulivyo na roho iko hivyo kwani moyo ni sehemu ya siri sana.Mungu huangalia sana moyo[ Sam 16:7], yanayo toka moyoni ndio yanayo kudhihirishia kama  roho iko utumwani au iko huru,moyo ndiyo imebeba chemchemi ya uzima ila uzima wenyewe upatikana katika roho ambayo uifanya nafsi kuishi [ mith 4:23].
Mawazo yako moyoni,ufahamu,hekima,upumbavu ,[mark 7:21].Hata kumpenda Mungu kuna takiwa kuanzie moyoni [kumb 6:5; zab 51:10] moyo ni kama nyumba huwa husafishwa ,mtu akimpokea Yesu ,Yesu anaingia  moyoni  mwake na kuisafisha kwa damu yake,  kwani baada ya moyo kuwa safi ndio roho  uweza kutulia.
Mungu huweka roho yake ndani ya  moyo  "ezek 11:19;36:26--27; zek 12:1. Kaa ukijua Moyo uokolewa na kusafishwa kwa Damu ya Kristo,laaakini roho ukombolela kutoka katika utumwa huko iliko tekwa na kufungwa,  kwani kwa adui huwa anichafua sana moyo wakati akimiliki na roho zake chafu kukaa humo, anichafua  hivyo  ili roho izidi kupata mateso,ilemewe na ikisha kosa uwezo wa kujitetea inatekwa,kufungwa  na kuanza kutumikishwa katika utumwa wa dhambi,kwa maana  dhambi huingia na kukaa moyoni hatimaye roho hulazimishwa kutenda  dhambi, hata kama roho ikitamani kutenda mema haiwezi kwani dhambi inakua imechukua nafasi kubwa sana moyoni mwa mtu  hivyo roho italazimika kutenda dhambi [ Rum 7:15--20].
Roho ya mtu ulitoka kwa Mungu hivyo huwa haiko tayari kutenda dhambi mpaka iwe imetekwa na kufanywa mtumwa wa dhambi na shetani huwinda roho ya mtu akiweka mitego yake kwenye milango ya nyumba yake  yaani moyoni[Mwa 4:7],katika moyo shetani hana uwezo wakuingia mpaka amepata mawazo ya moyo hii ndio lango kuu la moyo anaikamata na kuivunja.
Shetani anavunja lango hili kwani yeye ni Mwizi na hio ndio tabia yake [yoh 10:10]akiingia kwanza kabisa anakamata na kuharibu ufahamu, Shetani anakimbilia milango ya ufahamu kuu ya ufahamu na kuyamiliki ili mtu assijue kutofautisha lililo baya na jema , ana shika  macho na kuitia upofu tena aniwekea tamaa isiyo ya kawaida yaani ile mbaya,  anakimbilia masikio  ili mtu asisikie yaliyo mema na hata yakimfikia huyapindua na kuyafanya kuwa mabaya, ila anamruhusu mtu kusikia tu nakupenda kusikia yaliyo manajisi ili moyo uzidi kuchafuka.
Shetani anakimbilia mdomoni mwa mtu ili aweze kumlisha maovu kama maji na mtu kushiba dhambi tena kuona dhambi kuwa tamu na  kuitumia ulimi  kueneza sumu iliyomo humo moyoni ,kinywani anashikilia sana ulimi [Mark 7:21; Yak 3:5--8] akisha ushika ulimi basi hautuliziki tena ,utapata mtu anatoa matusi ,uongo na masengenyo na hata kutamka makufuru makubwa sana kwa kinywa chake, akishakuvamia na kuteka mawazo ndipo moyo ujaa dhami ila roho hutenda [Ezek 18:4].
Roho ya mtu haifi kifo cha hapa Duniani bali huishi kama Mungu aishivyo ,ila kwasababu ya dhambi itatupwa  katika moto wa milele kwa yule  ataye  mkataa Muumba wake.Mtu aliumbwa na moyo na roho safi isipokuwa alipata kuwa na  roho chafu alipo danganywa pale Eden.

ROHO YA WANYAMA  NA VIUMBE VINGINE

Kila chenye uhai kina roho kwani roho ndiyo inayo leta uhai na Mungu aliwapa  viumbe uhai kupitia roho wake  kwani kinacho watokea wanadamu inawatokea na wanyama vilevile ,wote wana pumzi moja[Mhub3:19--21;1Kor15:38--40].
Mungu anaweza kuwatumia hao wanyama kwa kutuma roho wake na kuwaingia roho ya hao wanyama kwani nao pia wana roho na hata shetani pia hutuma roho zake kuwainggia hao wanyama ili kuwatumia.Mfano mzuri tunaona wakati Yesu alipo toka majini baada ya kubatizwa na Yohana  mto Yordani [Math 3:16;Luk 3:21].
Shetani naye huwatumia roho ya hao wanyama kwani yeye ni mwizi wala hana chake ,anaweza kumwingia paka au mnyama yoyote na akamtumia,ndio maana hatakatika ndoto shetani anaweza kukuletea mfano wa mnyama kumbe anataka kutumia tabia ya asili ya huyo mnyama  ili aweze kukutesa nayo.

ROHO YA SHETANI [ROHO CHAFU]

Shetani  kabla hajawa shetani  yaani kabla ajawa mlaaniwa alikuwa malaika kama walivyo malaika wengine aliye kuwa akifanya katika ulimwengu wa roho ,ila akashindwa vita alio jaribu kupambana  na yeye aketiye juu,[Ufu 12:7Yoh 12:31].Roho za uovu,roho za dhambi,za uharibifu na roho ya mauti.
Yatupasa kujua kwanza roho za shetani yalivyo ili tuwe kuwa na uelewa tusije kudanganywa  nazo kwani kwa kuto kujua  mtu anaweza kujifariji kuwa anaroho wa Mungu kumbe  ni roho za shetani ,kaa ukijua kwamba hata shetani naye anaweza kujigeuza kama malaika wa nuru lakini sio nuru wala nuru haimo ndani yake . 
Roho za shetani zime gawanyika katika nafasi na nyanja mbalimbali za kiutendaaaaji kazi kama ifuatayo,hii ni kutoka kwa shetani mwenyewe  hata ngazi ya mwisho.
Ukitaka kufukuza roho za shetani ndani ya mtu sharti kwanza uweze kujua ni aia gani na ina fanya kazi vipi tena ikiwa ndani ya mtu anakuwa na tabia ya aina gani,tena ujue ina uwezo namna gani na ni mamlaka ya namna gani kwani huwezi kufukuza roho ya shetani bila wewe mwenyewe kujua utumie nguvu na upako wa namna gani wa kiroho kufukuza hiyo roho.
Kama ilivyo kwamba lazima ujue ni silaha ya namna gani ya silaha utumie ili kusambaratisha vifaru vyakijeshi  ata ukiwa mwanavita mzuri ila ukitumia bastola kusambaratisha kifaru nikama una chota maji ya Bahari kwa kutumia kifuniko ukiwa na leeengo la kuya maliza na kukausha Bahari,yaani ni kama unajisumbua bure.
Tuna shindana na falme [Efe 2:2  ;6:12b]hii ni mamlka ya juu sana ya kishetani kwani utawala na maelekezo utoka kwa mfalme ili famle wake uweze kujengwa na haaaina hii haikemewi ikaondoka  kirahisi kwani mtu anakuwa ana tumika  falme hio hivyo sharti kwanza mtum mwenyewe atolewe na kuingizwa katika ufalme wa Mungu na awe na ufalme wa Mungu ndani yake ndipo aweze kushinda huo ufalme na hata mtunishi wa Mungu sharti ajue kwamba hawezi kumtuo mtu katika ufalme wa shetani kirahisi mpaka yeye mwenyewe  yu na ufalme wa Mungu ndani yake .
Utashinda tu ukiwa na sauti  ya kifalme ,aliye kuhani wa kifalme awezaye kutamka kauli za kifalme.Huku ni kumtoa mtu katika  kuamini roho zidanganyazo na kuondoa kabisha habari za kuyaendea mashetani yaani kuwaendea waganga wa kienyeji,na kutumika huko.
Mamlaka ,hii ni ngazi ya mateso na kutawala kwa uwezo wa aina tofautitofauiti ,makandamizo yote yana patikana hapa ,kumilikiwa kote kunapatikana hapa huku ndiko hata wachawi wana pewa nguvu na uwezo huku mapepo na majini pia.
Huwezi kushinda wenye mamlaka kama wewe hauna mamlaka angalia lazima uhakikishe kama wewe unayo mamlaka juu yao na ili uwe na mlaka sharti uipate kwa Yesu na ili uipate hakikisha  uko katika kundi la wale anao wapenda  una weza kuwa na uwezo ila huna mamlaka,tena unaweza kuwa na nguvu lakini hauna mamlaka  [Math 28:18,].
Tena sharti uhakikishe kuwa unazo mamlaka  na nguvu na uweza tena kwamba vyote vimetiishwa chini ya miguu yako nawe waweza kuvitiisha vyote chini yako[ Efe1:20--22].                                                                                                                                                                                                                                                 
   Wakuu wa  giza ,hawa ndio roho zinazo husika na uchafu wote ule  kwani wanafanya kazi katika siri sana ibada zote za kuzimu na  za makaburini ndio ya nahusika hapa,hawamwachi mtu kujua kweli hata kidogo tena ,hawa wana wafanya watu wasiwe na macho ya kuona baya na jema kwao ni sawasawa tu,mauaji yote hupangwa huku ,habari ya uvamizi wote  upangwa huku  kwa wakuu wa giza[ luk 22:53]. Wakuu wa ngiza wanashindwa kwa kuachilia nuru [yoh 1:5].
Wakuu wa giza huwatuma wawakilishi wao hata katika nyumba za ibada na hata kujificha huko wakizidi kujificha huko kama walio wasafi kumbe giza  huwa wanatenda miujiza mingi ili kuzidi kuwapotosha watu.
Majeshi ya mapepo wabaya, haya ni makudi ya wapiganaji wa kishetani walioenea kila kona wakihaki kisha wana pigana na hao walio wanajeshi wa kristo wana weza kutembea kundi la kuanzia saba mpaka hata  maelfu.Wanashambulia kwa kasi sana japo pia kuondoka kwao ni rahisi lakini wanafanya kazi kwa kasi ya juu sana  waweza kuwa pata kokote na kumwingia mtu popote .
Lazima ujue namna ya kupigana vita katika maeneo haya kama Yesu alivyo fanya land force,upigane nchi kavu kwa ujumla palipo pagumu ni porini na misitu,milima na mabonde kwamba umepelekwa patakatifu au panajisi ." Bwana Yesu  alianza akamshinda huko nyikani akifunga siku arobaini[Math 4:1--11]. Kaa ukijua hata wakitoka kwamtu wana tembea nyikani pasipo na maji  [Math12:43;luk 11:24].
Alipo washinda kaika Gorrila war bush war wakakimbilia majini ,ndo hao majini unao wasikia [Math 8:31--33 ].Hawa ndio wanao simamia sana uasherati [2Nyak 11:7], " Akawafuata akiwa Marine komando ,walipomwwona wakataka kumwangamiza  na upepo na dhoruba akiwa na wanafunzi wake ,Yesu alinyanyuka akatuliza kwanza hizo gasia kukawa shwari [Mark 4:37--39].
Wakakimbilia chini ya ardhi huko kuzimu wakiwa na funguo,akaamua apigane nao humohumo kwenye maandaki !Under ground  war ndani ya siku tatu akiwa amekufa tena ifo cha msalaba ambapo walipo ona amesulubiwa wakashangilia wakisema amekwisha yule lakini ghafula mda wa saa tisa wakaona Dunia imetiwa giza wakachanganyikiwa kusema aliye kuwa nuru ame kwisha ,twendeni kule ni kwetu sasa wakaondoka kuja duniani na kumwacha bosi wao peke yake.
Yesu akasema sasa imekwisha akampiga mpaka kichwa kika gawanyika pande nne sawasawa kama msalaba ulivyo yenye maana Mwana kondoo amechukua ushindi wake pande zote za Dunia kwa damu yake na huyo mdanganyifu ameshindwa ,akamnyang`nya na funguo  ,akawafuata hukohuko kuzimuni  akawa piga nakuwa nyang`anya funguo akatupa sisi[Math16:18-19; 18:18; yoh20:23].
                     
Siku ya tatu wakati Yesu anajiandaa kutoka huko amechukua na baadhi ya mateka huko  shetani akatangaza kwa kilio kikubwa akiwaarifu  wanajeshi wake wakimbie ila wasishike njia ya kuzimu wasije wakakutana na Yesu kwani yuko njiani asije akawa maliza ,  ila wakimbilieni angani , "siwezi kuwasaidia tena kwani mimi nimesha pigwa sina mamlaka tena wala uwezo wa kupambana naye hata kwa sekunde.Ameshashinda kifo na mauti huyu  hatumwezi tena[Mdo 2:24-27]
Yesu akaja kweli Duniani wala hakuwa na haraka wao wakajifariji kwamba kweli huku hawezi kuja kwani alikaa siku 39 hajaonyesha kama anaenda huko lakini siku ya 40 kama alivyo piga ile ya kwanza siku 40 akiwa amefunga huko nyikani alipaa kwenda kupigana akiwa ni Airforce commando,wakashangaa nakusema tutaenda wapi bora tunyoshe tu mikono tumeshindwa [Mdo 1:9 ].
Mpango wa shetani kuzuia maombi ya watakatifu ikafutwa kwani Yesu alienda akakaa mkono wa kuume wa Baba akituombe tena yeye ndiye muombezi wetu mkuu anaye tuombea kwa baba[Heb 7:25; 1yoh2:1].

ROHO MTAKATIFU


No comments:

Post a Comment