Jukumu la tatu mwanadamu anapewa
akiwa katika shamba la edeni {mwanz 2:1,7-9,15} baada Mungu kumfanya mtu akampa
jukumu la kulima na kutunza lile shamba la edeni .tafakari haya!!
Mungu akamwambia alime-swala la
kulima inamaanisha kwamba ,aandaye shamba ,afyeke yaani kuondoa uchafu shambani
paonekane pasafi,apande mbegu yaote na tena apalilie yakue na kupendeza tena
yazae matunda.
Unapata kujua kwamba Mungu
alimweka huyo mtu kwa lengo la kuendeleza ustawi yaani awe
mzalishaji.Maranyingi watu wenye uelewa wana zalisha sio kuomba wapewe bali
wanatamani waweze kuzalisha ,hao wanaonyesha wazi kuwa wana yaelewa majukumu
yao ,jiadhari usiishi duniani bila kuwa anzisha kitu kipya ,wanyama wajue kuwa wewe unafanana na muumba
kwa kufanya mambo mapya katika dunia na
mazingira hayo unayo kaa kwani Mungu ni muumba na wewe umeumbwa kwa mfano na
sura ya Mungu, hivyo hakikisha unakuwa mbunifu tena ufanye jambo jipya kwa
ajili ya kuendeleza tabia ya uungu ya kiumbaji iliyomo ndani yako duniani
,onyesha unafanana na muumba wako.
Tatizo watu wengi hawapendi
kuumiza akili kutafuta mambo mapya ukisema neno teknolojia ni watu tu wamekaa
na kuumiza akili katika kutafuta wafanye nini
wapate mambo mapya ndio maana kuna ukuaji wa ujuzi na maarifa kuongezeka.
Kutunza maana yake kukifanya iwe
na asilia yake na muonekano uleule katka kuboresha na kufanyia marekebisho,neno
linguine hapa liwezalo kuelezwa hapa ni kwamba kulihifadhi kama unavyojua kuwa
wanyama nao walikuwepo hapo hivyo shamba ilitakiwa ikae ktk utaratibu maalum ya
kupendeza.
Ndugu mpendwa vitu vyite
vinahitaji matunzo ili yaweze kudumu katka uimara uleule kama ilivyo kua wakati
wa upya wake,jua ,nyota,mwezi bahari na upepo yana tunzwa kwa nguvu zake
mwenyezi ndio maana yanaonekana mapya kila wakati wala hazi choki tena
yanafanyakazi toka enzi hizo hata leo.
Watu wengi wasio na tabia ya
utunzaji manyumbani kwao hata kuwatembelea ni shida ,mara ukutane na sahani
mlangoni,kijiko kitandani nguo na chanuo au kitana juu ya ndoo ya maji,kwani
hata mke ,mume na watoto wanahitaji matunzo ,nguo ,gari,nyumba na kila unacho
kimiliki kinahitaji matuzo usije ukashindwa kutunza hatimaye yakwako yakisha
chakaa una tamani ya wenzako na kuyachukia kwani haujui kwamba unaweza
kumchukia mkeo ikiwa hana matunzo?
Ataonekana chakavu hata umbo lake
lime potea,tunza mazingira yako ,nyumba yako yafanyie ukarabati basi mpendwa
mbona yata onekana mapya tu ,tena masafi hayo Mungu anatuangalia kama tuta kuwa
watunzaji ili atuamini na kutu patia yaliyo mema zaidi.
Hata wokovu unahitaji matunzo
kwani tusipo utunza hatuwezi kupona[hebr2:3},uponyaji unahitaji matunzo,miujiza
inahitaji matunzo ,karama za rohoni zina hitaji matunzo.Kwamaana anayetunza
anajali akiyunzacho,anakithamini,anamweshimu aliyempa na kukiheshimu kitu
chenyewe,anakilinda kile anachokitunza na anakiangalia na kukikagua kila wakati
ilikuhakiki usalama wa kitu hicho.
Tusidanganyane mpendwa ukionawewe
vitu vyako nyumba yako kila unacho kimilika hakina matunzo wewe hata kuingia
uzima wa milele sio rahisi kwa maana ikiwa unashindwa kuyatunza vitu vya dunia
hii viaharibikayo utaweza kutunza moyo wako ?na vipawa vya roho uta viweza?
Jukumu la nne aliyo pewa mwana
damu nipale kuya tambua mawazo ,kujua tabia ya wanyama na ndege ili kuwapa
majina na kuwapanga katika nafasi zao kila mnyama na kila ndege kwa jinsi
yake.Mungu hakuja kuwapa mjina hao ndege na wnyama bali Adam ndiye aliye pewa
jukumu hili na akafanya kama kiongozi{mwan2:19,20} .Ndipo alipo pata baadhi
yawanyama wakufugwa na wengine sio wakufugwa yaani wa mwituni cha kushangaza
jina alilo mpa mnyama huyo ndilo lilikuwa jina lake.
Nimalize kipengele hichi kwa
kusema:
KILA KIUMBE NI MTUMISHI WA MUNGU.
Ndugu mpendwa utaelewa nakukubali
kauli nhii kwani viumbe vyote vinamtumikia Mungu kila kiumbe kwanamna yake na
nafasi yake ,kwa maana katika uumbaji hakuna kilcho umbwa kwa bahati mbaya bali
kila kiumbe kwa kusudi maalum hata wale ambao wewe waweza ona kama hawana faida
kwa Mungu wanafaida na thamani kwani aliviumba wafanye mapenzi yake ,kila jambo
kwa kusudi jin ya jua [
Mhub3:1} usione hicho unacho kiona
ukasema kipo ahpo kwa bahati mbaya usimkosoe Mungu ndugu yangu .Hebu tuangalia
ni kwa namna ganiviumbe hivi baadhi vinavyo mtumikia Mungu kwa kutenda mapenzi
yake{inathibitika kuwa viumbe vingine tofauti na wanadamu wana ya fanya sana
mapenzi ya Mungu katika kutimiza bila kukosa kufanya hivyo hata siku moja wala
hawahitaji usimamizi.
Juan a,nyota,mwezi,upepo,maji ya
bahari,nchi,mimea, hawa ni mifano bora kabisa.
Jua ambayo kazi yake ni kuipa
dunia mwanga (nuru)na joto huchomoza kila hasubuhi na kuzama jioni hakuna anaye
msimamia tangu ilipopewa kazi hiyo ,mwanga huu wa jua unahitajika na wanyama
ili waweze kuona waendako na kufurahia dunia jua likizama utashangaa hata kuku
wa kwako wanaingia ndani kupumzika waisubiri tena kesho yake.
Mimea huhitaji mwanga wa jua ili
waweze kutengeneza chakula cha kupitia majani yaon ,utaona mti ukiota majani
yake uenda juu kutafuta mwanga wa jua hata ukijani ya majani utegemea jua kwani
majani yakikosa mwanga wa jua majani hukosa
rutuba na kupoteza uasilia wake tena uanza kuwa wanjano.Tena ili mbegu ya mimea
iote inahitajika joto la jua kiasi.
Wanyama nao miili yao uhitaji joto lajua ili miili iweze
kuchangamka,na damu kuweza kutembea vizuri ktk miili yao ,baadhi ya wanyama
pamoja na kwamba wana weza kudhuru lakini wanashindwa baridi ikiwa zidi ,mfano
nyoka :utampata amejikunja kujinyoosha anashindwa mpaka apate joto ,nyigu na
nyuki nao hawawezi kukungata wakati baridi imewazidhata I miili yao,bila
kusahau mwana damu ambaye ndiye mtumiaji mkubwa wa mwanga wa jua na joto lake
utapata wanatafuta vitamin D na wakikosa wanapata ugonjwa ,kwa ujumla utaona
hasubuhi wanyama wanatoka nje kutafuta jua !hivyo kwa namna hii jua umtumikia M
ungu na kutimiza kusudi la kuumbwa kwake.
Upepo –wote twajua kuwa upepo
nipumzi ,hapa ndipo penye uhai wa viumbe hai wote “tuna soma bwana Mungu
akamfanya mtukwa mavumbi ya ardhi na kumpulizia pumzi ya uhai binadamu akawa
nafsi hai{mwa 2:7},upepo huo huenda baharini nakudumisha uhai wa samaki,wanyama
wote ,mimea nayo kwani upepo uvumapo hiyo pumzi iliyoko ndani hutoka unapo
pumua na unpata hewa safiiii!.Ukiwekwa mahali hakuna hewa yaani pumzi unakufa
sio mda mrefu.
Upepo uvumapo baharini huchukua
mvuke nakuenda nayo juu tena huyapeleka na nguvu yake ,yakifika juu huyapa
baridi hata yana ganda kuwa barafu hapo pia bado huya sukuma,yakiyeyuka kwa
msaada wa huyasukuma na kuyapeleka
sehemu mbalimbali juu ya nchi sehemu isiyo na maji,mvua unyesha na mimea kuota
wanyama wanapata chakula .Tena kwa kubeba mvuke huipooza nchi pale joto la jua
linapo zidi kwani ikiwa upepo una vuma najua inawaka utasikia ukali wa jua una
pungua.
Bahari –samaki na wanyama wengine
wana makao yao humo humo baharini wakitolewa tu baadhi kama samaki hawawezi
kuishi ktk nchi ,wanyama nao wanatulizia kiu yao huko.kwaujumla maji ni sehemu
ya uhai asilimia kubwa ya miili ya viumbe hai ni maji.
Nchi imehifadhi vingi hata sisi
tunaishi juu yake ,ndege baadhi ya wadudu na wanyama wanaishi juu ya ardhi
mimea pia ardhi tuita mtetezi wa maisha.Vyote vina fanya kazi maalum kulingana
na maagizo ya Mungu.
Baada ya Mungu wetu kuiona roho
yake namna alivyo tulia juu ya vilindi maji akaona hakika nimeiona sura yangu
mwenyewe inavyo pendeza juu ya dunia hivyo hivyo kazi ya umbaji uliendelea
lakini huku Mungu amesha ona sura yake na mfano wake ni nzuri sana
ikimwakilisha duniani.tunasoma nayo nchi ilkuwa ukiwa na roho ya bwana Mungu
ikatulia juu ya uso wa maji (mwanz1:2)
Tunapo sema roho ya Mungu
tunamsema Mungu mwenyewe yaani nikama yale maji yalikuwa kio yakujitazama sote
twajua kuwa Mungu wetu ni roho (yoh4:24).viumbe vyote vilihitaji uongozi ndio
maana binadamu aliumbwa.
MTUMISHI KIONGOZI
Sasa ninapo sema mtumishi kiongozi
nilazima tujue kuwa watumishi wa Mungu tupowengi lakini lazima kuwepo maongozi
na madarajaya kiroho ili kazi ya bwana itendeke kwa ukamilifu ma utaratibu
uliyomzuri kwani ndivyo ilvyo hata mbinguni,sisemi wewe sio mtumishi wewe ni
mtumishi lakini sio wote tuna teuliwa kuongoza, hii kazi ni kubwa tena ina
idara nyingi ,tunasoma hata wakati ya mitume kundi ilivyo ongezeka kazi ilkuwa
kubwa hata idara zote zikawa zinalemewa “ndugu haipendezi kuliacha neno la
Mungu na kuhudumu mezani ,chagueni watu saba miongoni mwenu,muwaweke juu ya
jambo hili nasisi tudumu ktk kuomba na kulihudumia neno {mdo6:5-9} .Hatuwizi
wote kuwa daraja moja hapana ,Mungu wetu
ni wa utaratibu, lazima kuwepo na nidhamu imempasa Mungu kuwa chagua wengine
miongoni mwetu kuwa viongozi ,tunaona hata kipindi cha musa ,alimchagua joshua
wakiwa na haruni kuhani tena akawachagua wengine {kuto18:25-26;kum1:15-17}
Mungu hawezi kusema na wote bali Munguwetu anapenda sana kumchagua mtu ili
kusema naye kuhusu watu wake ,atamuonyesha njia ,kumjulisha siri nao watafuata,
atamwonyesha njia bali yeye atawachagua watu wa aina Fulani kama roho mtakatifu atavyo mwelekeza na kama Mungu
apendavyo.
Ndugu mpendwa nivyema tuangalia
makanisa ya leo yamejaa wana wa uzao wa kishenzi ,wakifika tu kwenye huduma
ambayo hata Mungu hakusema nao wala hawajui alifanya agano ya namna gani na
huyo mtu ,utasikia na mimi pia nina maono hacha upumbavu mwana wa uovu Mungu
angekuona bora au angekuona unafaa angekuweka kwani unataka kuniambia yeye
hakukuona.utasikia mimi huko niliko toka nime achakanisa kubwa nililo lianzisha
!wewe uongo tu Mungu hawezi kukuchagua na kukupa kundi lake halafu wewe unasema
umewaacha wao wana chungwa na nani? Wewe umesha shindwa kazi mwana wa uharibifu
,huwa wanatafuta nafasi waweze kuharibu .
Cha ajabu wanaanza kuwa sumbua
watumishi wakisema “nasikia moto wa injili mchungaji tupatie vipindi tuweze
kuhubiri,kwani moto wa injili ikikushukia unataka uwahubiri watu kanisani
haujui humo wapo ambao tiyari wamekombolewa kutoka huko waliko kuwepo nje
dhambini,tayari unaona wanamwabudu Mungu wao humo,wapendwa kanisani sio sehemu
sahii ya kuhubiri ila ni mahali ya ibada,tena waliomo kanisani wanatakiwa tu
wafundishane ,wewe nenda huko nje wako wenye dhambi wengi hawajaokoka ,katafute
kondoo walioko nje acheni ujinga.
Usidhubutu kabisa kumdharau
mtumishi ambaye unaona amesimamisha kazi ya Mungu hata kama unajua kuhubiri
kuliko yeye ,unajua kuomba au kufunga kuliko yeye wewe mwache acheni kuwasumbua
watu waMungu kwani akiharibu ni juu yake na huyo aliye mtuma.usiendekwa akili
zako,huduma nyingi zina pata shida na kugawanyika kwasababu kila mmoja alitaka
kuleta maono yake Mungu hasemi na watu wote juu ya kundi moja bali atasema na
mmoja yule aliye mpa dhamana ya kuongoza kundi hilo.
Hii iliendelea mpaka alipo kuja
Yesu tunasoma”Naye aliwatoa wengine kuwa mitume ,na wengine kuwa
manabii,wainjilisti,wachungaji,waalimu{efes4:11;1kor`12:28-31}.Cha ajabu ni
kwamba huduma nyingi hawatambui na wala hawaja jua namna ya kupanga madaraja ya
kiroho kulingana na vile roho mtaka tifu anavyo gawa karama na kuziweka huduma
ndani ya kanisa. Leo hii watu wanaenda tu wakisha soma huko chuoni basi kulingana
na daraja la kusoma biblia wanapangiana vyeo ajabu hii,hata imefikia
wameibadilisha taratibu ya roho mtakatifu nakujiwekea wenyewe yaani wanapanga
wadogo kuwa juu ya wakubwa wao.
Kanisa la leo lime poteza mwelekeo
,sikuhizi mtu akijua kusoma biblia tu anaendachuo akitoka huko utasikia tunaye
mchungaji mpya amevuzu masomo yake juzi na ana digrii yake, ninacho jua mtu
anaitwa,anaitika ,anamfuata aliye mwita,akimtuma na atamwambia nakutuma nini
wapi,na kwa nani.Ninacho shangaa sikuhizi utasikia heti kaigiza kwenye filamu
na sasa anagombea uchungaji haya nimaajabu watu wako kimwili zaidi.yaani wana
gombea siku hizi kama vile wabunge poleni sana ngoja atakapo kuja mwenyewe
mtaona atakavyo wafanyia haswa wanao jiita ni watumishi wake na huku
hajawatuma.
Utasikia wengine kanisa inalipa
hivyo wana fungua ilikufanyabiashara wapatefedha ,kizazi cha uovu ,wenye tamaa
na kujipenda wenyewe Mungu mwenyewe ansema hajawatuma bali waliondoka na kwenda
wenyewe hakusema nao{yer23:16,21,32:} ,wanafiki wakubwa wameacha kuhiubiri
ukweli wa Mungu na ufalme wake wakahubiri maslahi yao ili wapate mali,wame kuwa
ombaomba wakililetea tusi jina labwana{tito1:11}. Wengine husema nimeitwa je
uliitika? Kama uliitika umemfuta na kumsikiliza?alikuitia nini? Kama umetumwa
!ni wapi kwanani ,ukapeleke habarigani au ukafanye nini ?je ndio mda
aliokuambia sasa nenda? Amekuambia weweunaenda kama nani? Kunbuka alikutana
naAbraham akambadilisha jina kuwa
Ibrahim{mwan baba wa mataifa {17:5},sarai akambadilisha jina kuwa
sara{mwan17:15} ,alipo kutana na Yakobo alimbadilisha jina akaitwa
Israel{mwan32:28;35:10},alipo kutana na sauli akambadilisha jina akawa
Paulo{mdo 13:9}
Wapendwa kazi hii ni ya heshima
kwelikweli haihitaji kuvamiwa hivyo tena yagharama ilimgharimu Yesu uhai
,usiwaone watu wameokoka kuna gharama kubwa sana mpaka waokoke.
DHAMANA YA MTUMISHI KIONGOZI KANISANI
Kanisa la yesu kristo lilipangiwa
taratibu maalum ya kukamilisha mwili wa kristo ambalo ndilo kanisa lenyewe,mimi
naongea na kanisa wala sio dhehebu wala dini, mimi sifundishi mambo ya dini
hapa ila nayafundisha mafundisho yanayo husiana mwili wa kristo ambayo katika
mwili huo mimi ni kiungo moja wapo tena kiungo kionekayo kuwa ndogo.Ninapo sema
kanisa siongelei hekalu au majengo ya kuabudia ,bali naongelea mwili wa kristo
abayo pia ni kundi la wale aliyo wa komboa kwa damu yake.
Watu wengi wamejiita kuwa wao ni
wakristo ,nikuambie kwamba ukriso sio dini ,wanaoitwa wakristo ni wale
waliokombolewa wewe kama unaona hauja okoka na unaenda kanisani ukijiita
mkristo unajidanganya mpokee kwanza awe bwana na mwokozi wako ndio uwe
wake,heti wenye dhambi na wana wa uovu husema sisi ni wakristo wakati
hawafanani naye hata kama unasali na waliokoka na kuimba kwaya wewe sio
mkristo,we haujishangai kwamba yeye aliye wake amewpa uwezo kuwa wana wa Mungu
nao hawatendi dhambi wako kama babayao{1yoh3:7-9} wajiita mwana wa Mungu uzao
na asili yako ni yakishetani imeandikwa atendaye dhambi ni wa ibilisi.
Watu wangejua kuwa hawarusiwi
kulikiri jina la kristo wala kutangaza habari zake {1 tim2:19} kila akiriye
jina la bwana sharti atengane na uovu,bali mtu asiye haki Mungu humwambia !
bali asiye haki Mungu humwambia unanini kutangaza habari zangu na umeyachukia
maonyo,uliyatupa maneno yangu nyuma
Mtumishi kiongozi mimi
nitakufundisha kulingana na Yesu alivyo panga maongozi ktk kanisa kwahiyo
watumishi viongozi ni hawa,{efes 4:11;1kor12:28-31}.ndugu mpendwa naomba tu
unielewe kwamba ninapo sema mtumishi kiongo,watumishi viongozi naongelea wale
ambao wanaangukia au wamo ndani ya huduma kuu tano ya maongozi sio karama
kumbuka stefano hakuwa kiongozi bali alikuwa na karama ya miujiza akatenda
maajabu makubwa hata wakamua{mdo6:8;7:59}.
Hawa ndio watumishi viongozi
mitume,manabii,wainjilisti,wachungaji na waalimu,ila leo naona watu
wamebadilisha wanasema wakwanza ni askofu na wapili mchungaji halafu wanaishia
hapo ,utamsikia mchungaji asite na akili na wala hajui neno na madaraja ya
kiroho akitaka kuwapotosha watu kwa kuwaaminisha kwamba yeye ndiye mkubwa
,wanasema m,itume hawapo eti ilisha nyakati wa paulo,na manabii waliishia
nyakati wa yohana ! kama unsoma somo hili sioni aibu kukuambia kuwa wewe ni
mpumbavu na wala hamsikilizi roho wa Mungu aliyeko ndani yako, kwanini wepo
mchungaji asiwepo nabii au mtume,nikuambie askofu hata ktk karama askofu hayupo
wala haja tajwa inakuwaje amzidi hata mwinjilisti?ndio maana kanisa siku hizi
haina mamlaka wachawi wanawaangusha wachungaji madhabahuni kwani kaka yake
hayupo kwahiyo hata shetani anawaonea tu.
Huduma maongozi yakikosekana
hatakupanga vipawa sio rahisi na ninachojua nikwamba sirahisi mchungaji kuelewa
ikiwa roho amempa huduma hiyo kanisani humo kwa kuwa ni kaka yake utasikia
akiuto huo unabii moyo wa mchungaji unamsumbua na kufikia kumkufuru roho
akisema hakuna cha mungu kasema hapa!.
Hauwezi kutaka kuwa nabii wala mtume bali roho ndiye anaye kujalia kuwa
hivyo maumivu na mapito ya huduma hizi sio madogo,uaskofu unaweza kutaka na
ukafanya siniungalizi tu wa kundi la mungu{1tim3:1-14}halafu kunasifa zake za
kuwa nayo ukiwa nazo tu basi unaweza ila paulo akiwa hana mke tena aliye kuwa
muaji Yesu akamteu awe mtume kazi ngumu kweli sitaki kabisa uamini kuwa askofu
ni mkuu japo umefundishwa hivyo na dhehebu lako.
Dhamana ya kulinda kundi(
kondoo)yoh17:12 walinde wakati ukonao yakwamba wako safarini au wako hapohapo ,walinde
kwalile jina ulilopewa yaani jina la Yesu {mdo 4:12} ,walindi dhidi ya maadui
,mbwa mwitu,wadanganyifu,wapotofu ukiwa fundisha wamjue Mungu bab na Yesu
kristo aliye mtuma{yoh17:3;8:32} wasikimbilie huku na kutafuta miujiza kwa yesu
aliye kuja kutoka nchi za jirani.
1.
Dhamana ya kuwaokoa na
maadui,hatari,maangamizi,kubali kuhatarisha maisha yako ili kuwaokoa wao,paulo
anasema heri afe {1kor9:15},jinyime haki yako ya kulala,kula ,kufurahi
,kuheshimiwa ili wao wawe salama.Tunamuona Daudi akitupa mfano bora kweli yeye
wakati anchunga kondoo wa baba yake alihatarisha uhai wake mbele ya simba na
dubu ili kuokoa kondoo{1sam17:34-37},anasema simba akimkamata kondo namkimbiza
akini rukia namshika ndevu zake nakumua.
Dhamana yakutafuta walio
potea,wachungaji wengi watu wanapo potea hawaangaiki ,tena hawaendi kuwahubiria
watu huko nje wamjue yesu wanataka wahubiri waliomo kanisani walio kwisha okoka
hao wanahitaji kufundishwa tu ,usikubali watu kutoka mkononi mwko hivi hivi
mtumishi wache hawa ulionao wao wako salama kamtafute yule aliye
potea{math18:11-14;yoh10:11,52;luk 15:4-24;ezek34:16}.
Dhamana ya kuwa ganga na kuwatibu
majeraha yao,wengine wamevunjika ujue huko waliko kuwa wamepitia mengi na
kuumizwa na mengi wengine mbwa mwitu ,dubu,simba ,mbweha na wanyama wenine
wakali waliwakamata nao wameponyeka kidogo waliwe jua wana majeraha wakague
vizuri,wengine wanavuja damu kwandani mwambie roho mtakatifu awapige x-ray na
kukuandikia dawa ili wewe uwape wapone,{isay61:1;yer23:4}.usiwekiongozi
mpumbavu {zek11:15;eze34:2-12}.Wote twajua kuwa wako wachungajiwanao haribu
kondoo wa malisho ya nyumba ya bwana ni mambo yakusikitisha wachungaji wengine
wametenganisha ndoa za watu ,wamezaa na wake za watu ,wengine wamewabaka yaani inaumiza roho
kweli{yer23:1-2;zek11:4-5}.
Dhamana ya kuwapanga ktk nafasi
yao kila moja kwajinsi yake,nivyema Mungu akupe kujua wale unao waongoza ili
ujue kuwaweka ktk nafasi zao bila hilo kazi inakuwa ngumu,usimweke mtu
ktknafasi isiyo yake kwani hataweza kufanya hiyo kazi,lazima uje kuwahukumu wale
ulionao elewa kuwa kondoo wengine ni wachanga,wengine wana mapembe makubwa
waweza kuumiza wenzao,wengine wanamimba ,wengine ni wagonjwa wengine wanaafya
nzuri,wengine wamekonda na wengine niwanene !ukiwachanganya pamoja wote hawa
kundilitakuwa na vilio na matatizo makubwa.Wengine hawajui kula kiustarabu
wakisha kula hukanyaga yalio salia kwa miguu ndio wale wanao watukana na
kuwadharau watu mishi wao,wengine wakorofi wengine wapole{ezek34:18-22}. Hao wakorofi na wenye mapembe wasije wakawa
jeruhi na kuwa umiza wenye mimba ukakosa kondoo hao watoto wao na maziwa pia.
Dhamana ya kuwatuo nakuwapeleka
nje ili kuwapa malisho mazuri,nakuwanywesha maji masafi,wapate majani mabichi
na maji ya utulivu,tena hakikisha wanashiba,angaika ili wale vizuri leo kuna tatizo
la kondoo katangatanga huku na huku tena wanavamia mashamba na kufikia htua
yakuuwawa na wenye mashamba hayo mbali.utaona wakivumilia njaa hiyo sana
wataanza kupiga kelele na kukuvunjia heshima kwani hapo ndipo wachungaji wanapo
anza kudharauliwa na kundi wanalo ongoza na kusababisha laana ktk kundi nzima.
TAHADHARI KWA MTUMISHI KIONGOZI
Jitunze nafsi yako na lile kundi
lote ambayo roho mtakatifu ame kuweka uwemwangalizi juu yake{mdo20:28)
Jihadhari uifanye kazi hii kwa
moyo wala sio kwakutaka fedha{1pet5:2-4yoh10:12;tito1:11}.
Dumu ktk mafundisho ukijitunza ili
kujiokoa pamoja na wale wanao kusikiliza pia{1tim4:16}.
Usiwe mwepesi wa kuwa pendelea
watu au kuwawekeamikono ,au kumhudumia mtu msikilize kwanza roho
mtakatifu{1tim5:22}.
Uweze kukaza kumpenda kristo ndipo
utapo kuwa naupendo na hao alio wanunua kwadamu yake ,alipo taka kumkabidhi
petro kazi alimuuliza kama anampenda sio kama amekomaa ki imani{yoh21:15-17}.
Mungu akubariki na kukuimarisha
uifanye kazi yake kwa athabiti kabisa ukiwa na uelewa katika yote yanayo
kupasa.
Namshukuru Mungu baba ,Yesu kristo
na roho mtakatifu kunifunulia siri za mbinguni.
PRE:BY TEACHER OCHIEN”G
OMENO{9|03|2015 PHONE 0688390634
No comments:
Post a Comment